Select Menu

Slider

Powered by Blogger.

Music

Health

Sports

News

Photos

Documentary

Video

 Kuna hii biashara ya mahindi ya kuchoma (maarufu kama gobo). Unaweza kulima kwa kutumia mtaji kidogo na kupata sarafu za kutosha. Angalia mchanganuo ufuatao: kukodi shamba ekari moja wastani wa tsh 50,000/=, kulima 30,000/=, kupalilia 30,000/=, mbolea mifuko mi-3, tsh 150,000/=, madawa wastani tsh 50,000/=; Jumla kuu ni tsh. 310,000/=. Gharama hii hauitoi mara moja bali ni kidogo kidogo kutegemea hatua husika. Mahindi huchukua wastani wa siku 90 (miezi mitatu) tangu kupanda hadi kugoboa (yaani kuvuna haya mahindi mabichi). Unaweza kupanda kwa kutumia mvua au kutumia umwagiliaji mahali popote Tanzania. Kwa ekari moja ukilima kwa kuzingatia utaalamu una uhakika wa kuvuna kuanzia mahindi 9,800. Hindi moja huuzwa kwa tsh. 150/= hadi 250/=, kutegemea hali ya soko kwa bei ya jumla. Ukikokotoa utaona kuwa kwa ekari moja unaweza kupata tsh. 1,470,000/= kwa kadirio la chini na tsh. 2,450,000/= kwa kadirio la juu. Ukitoa gharama za uendeshaji (za moja kwa moja) unaweza kukunja faida ya hadi tsh 2,140,000/= kwa kadirio la juu. Ukilima eka 5, una uhakika wa faida ya tsh milioni 10.7. Je, ukilima misimu kadhaa, bado utashindwa kujenga nyumba ya maana au kuwa na maisha yenye unafuu? Bila shaka utaweza! Unachohitaji wewe ni mambo yafuatayo: utayari, uthubutu, kuwa-up-to-date kwa taarifa za misimu na masoko na uwe ni mtu wa kufuatilia fursa na kujifunza. Fursa zipo 'bwerere', kama una 'allergy' na kilimo tafuta na ujifunze fursa nyinginezo; LAKINI; mtu YEYOTE anaposema fedha ni ngumu, kiukweli anakuwa hayupo "serious" kabisa na haya maisha! http://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js

 HIVI ndivyo anavyosema mkulima wa nyanya kutoka katika kijiji cha Mangalali, bwana Paschal Sichalwe baada ya kuanza kubadili mbinu za kilimo za kizamani na kuanza kutumia mbinu za kisasa alizozipata kupitia mafunzo yanayotolewa na mradi wa Muunganisho Ujasiriamali Vijijini (MUVI)
http://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js

Mjasiriamali huyu mdogo anaelezea namna ambavyo mradi wa MUVI ulivyoonesha njia ya kuelekea kwenye mafanikio kwa kutoa mafunzo ya kilimo bora, kuboresha njia za mawasiliano baina yao pia jitihada zinazofanywa katika kuwaunganisha na masoko mbalimbali ya ndani na nje ya nchi Mradi wa MUVI kwa kushirikiana na viongozi wa shirikisho la wakulima wa nyanya wamefanya ziara za ndani na nje ya nchi katika harakati za kutafuta masoko zaidi, katika hatua za awali uongozi huo umefika nchini Kenya, Malawi na hatimaye Zambia hii ikiwa ni kwa upande wa masoko ya nje Masoko ya ndani, mradi wa MUVI ambao pia umeimarisha kitengo chake cha biashara na masoko wameangalia masoko ya ndani ya nchini na kugundua kuwa kinachosababisha nyanya kushuka bei ni kukosekana kwa taarifa za biashara na masoko kutoka katika ngazi zote. Katika kutatua tatizo hilo tayari mtandao wa mawasilano kutoka mikoa yote Tanzania zitakuwa zikipatikana ili wazalishaji wa nyanya waweze kufahamu soko liliko. Wakulima wanapopata taarifa za biashara na masoko inakuwa rahisi kwao kufanya maamuzi ya soko. Pia matumizi ya mbao za matangazo kwa kushirikiana na redio country fm88.5 fm na Uplands redio 89.0 fm wajasiriamali vijijini wataweza kupata taarifa za biashara na masoko. Aidha bwana Sichalwe ambaye ameanza kuvuna nyanya alizopanda kitaalamu akitumia mbegu bora aina ya Eden inayozalishwa na Kampuni ya Monsanto anasema kuwa ameanza kuona faida kwani mara ya kwanza ameweza kuchuma tenga 33 ilihali msimu mzima uliopita katika shamba hilo hilo lenye ukubwa wa nusu ekari kwa ujumla alivuna kiasi cha tenga 56 tu. “Msimu uliopita nilitumia mbegu aina ya ONXL katika shamba la nusu ekari michumo yote nilipata tenga 56 tu lakini sasa mchumo mmoja nimewezakuchuma tenga 33 na nategemea kuchuma kiasi cha tenga 26 katika mchumo wa pili.” anasisistiza Sichalwe. Msimu uliopita nilitumia kiasi cha shilingi 532,800 ikiwa ni gharama nzima ya uzalishaji kwa upande wa pembejeo pamoja na nguvukazi,mapato ilikuwa 606000, msimu huu nimetumia kiasi cha shilingi 570,900 kwa ajili ya pembejeo na nguvu kazi nategemea kupata kiasi cha shilingi 1,045,000 Kwa mtizamo wa haraka haraka, bwana Sichalwe ameanza kuona faida katika kilimo cha nyanya kufuatia mchanganuo huo alioufanya. Sichalwe ambaye pia pamoja na zao la nyanya hujishughulisha na kilimo cha alizeti na mahindi, katika hatua nyingine amewezakuimarisha biashara ya kuuza bidhaa ndogondogo kwenye kibanda chake ambapo pia anaamini kuwa kuna siku atakuwa mjasiriamali mkubwa. Awali Sichalwe alikuwa akilima kwa mazoea bila kutunza kumbukumbu kuanzia uzalishaji hadi sokoni lakini baada ya mradi wa MUVI kupisha hodi kijijini kwake na kufundishwa kilimo cha kibiashara na njia rahisi ya kuandaa mpango biashara sasa ameweza kutunza taarifa zake za kilimo tangu hatua ya mwanzo hadi mwisho, hapo ndipo anapoweza kubaini mapato na matumizi katika shughuli nzima. “Wajasiriamali wengi wanasahau kuweka kumbukumbu za uzalisha katika shuguli zao wanazofanya kila siku, mali bila daftari hupotea bila kujua,kila unachofanya inakupasa uandike, kuna wengine pia hujisahau wao wenyewe, mfano akipalilia nyanya mwenyewe au akipanda hujisahau katika kipengele cha malipo ile ni nguvu kazi inapaswa kulipwa na hili linawezekana kama utakuwa umeandika”anasema. Katika hatua nyingine Sichalwe anaamini kuwa baada ya kupata mavuno mengi na yakutosha msimu huu anatarajia kuanza kilimo cha umwagiliaji ambacho anaamini kuwa kitamkomboa zaidi. Pamoja na mambo mengine Sichalwe anampango wa kuimarisha kilimo cha ufugaji kwani tayari amenunua mbuzi 5 mara baada ya kuuza nyanya. Idadi hiyo anaona kuwa haitoshi hivyo anategemea kuongeza kiasi hicho hadi kufikia mbuzi 20. Si hapo tu Sichalwe anaamini pia kwa kuzingatia mbinu za kisasa alizozipata kupitia mradi wa MUVI kufikia mwishoni mwa mwaka atakuwa amenza ujenzi wa nyumba ya kisasa ya kuishi. Katika kuhakikisha kuwa Sichalwe na wajasiriamali wengine wanaozalisha nyanya kijijini hapo wanapata mafanikio, mradi wa MUVI umemtuma ofisa masoko wa mradi huo kuzungumza na na wakulima wa nyanya katika hali ya kuwaondoa hofu hususani kwenye kipengele cha masoko. Akizungumza na wajasiriamali wa Mangalali hivi karibuni muda mfupi mara baada ya kuunda kamati ya biashara na masoko, Ofisa masoko wa mradi, bwana Fredy Mumbuli amesema, wakulima wanategemea zaidi soko la Kariakoo na Ilala.Wafanyabiashara hawa huwa wanakimbilia katika masoko haya kwa kukosa taarifa nzuri za masoko. “wajasiriamali hupeleka nyanya kwa wingi katika masoko hayo kwa kukosa taarifa sahihi za masoko hali inayoplekea kushuka kwa bei ya bidhaa husika,wakulima wote nchini wakishavuna hufikiria kuuza bidhaa zao Dar es salaam jambo ambalo si sahihi hata kidogo.”alisema Mumbuli. na kuzidi kubainisha kwamba kuwa kuna wakati kunakuwepo na uhitaji mkubwa wa nyanya Morogogo, Arusha au Dodoma na hata wakati mwingine Iringa Mkulima anayezalisha nyanya Morogoro akipata taarifa za soko zuri la nyanya Iringa anaruhusiwa kufanya biashara vivyo hivyo na kwa upande wa mkulima wa Arusha, Kilimanjaro na mikoa mingine inayolima zao hilo. Hili litawezekana mara baada ya kuimarisha njia za upashanaji habari kupitia vyombo vya habari na mbao za matangazo ambazo tayari mradi wa MUVI umejenga katika kata 16 mkoani Iringa na Njombe. Kitengo cha habari na mawasiliano kitakuwa kikifanya kazi kwa ushirikiano mzuri na kitengo cha biashara na masoko katika kuwapatia wakulima taarifa za biashara na masoko.

KUKOSEKANA kwa wataalam wa ugani na zana bora za kilimo imekuwa ni changamoto kubwa inayomkabili mkulima wa ufuta jimbo la Chalinze mkoani Pwani. Ufuta ni zao la biashara ambalo limeanza kulimwa kwa wingi katika mkoa wa Pwani,hasa jimbo la Chalinze kutokana na soko lake kuongezeka kila msimu. Zao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara,mbegu za zao hili huwa na wastani wa mafuta kiasi cha asilimia 45, hata hivyo wakulima wake wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa nyenzo na elimu. zao hilo limeanza kulimwa kwa kasi katika miaka ya hivi karibuni katika eneo hilo baada ya soko lake kuongezeka kutoka sh.1000 kwa kilo miaka mitatu iliyopita hadi sh.2800 kwa kilo. Hata hivyo licha ya wakulima wengi waliokuwa wamekata tamaa na kilimo cha mahindi kuamua kuingia sasa shambani kulima ufuta wameanza kukabiliana na changamoto nyingine. Katika baadhi ya maeneo hususani kata ya Lugoba watalaamu wapo lakini wanadai kuwa hawana usafiri wa kufika kwenye maeneo ya wakulima kila mara ili waweze kutoa elimu inayotakiwa kwa wakati muafaka. Awali wakulima wengi walikuwa wamesusa kilimo cha mahindi kutokana na kukosekana kwa mvua za kutosha, zana za kilimo na mazao kuharibiwa na mifugo. Hali iliyochangia ugumu wa maisha katika jimbo hilo na njaa za mara kwa mara lakini sasa baada ya wakulima kugeukia kilimo cha ufuta ambacho wanaamini kuwa mazao yake hayasumbiliwi na wanyama kama ng’ombe maisha yameanza kubadilika. Kutokana na kukosekana kwa zana bora za kilimo kama matrekta au jembe la ng’ombe wakulima wamekuwa wakitumia mkono hivyo kuambulia kulima eneo kidogo nakushindwa kujikomboa. Felex Butahe ni mkulima ambaye ameanza kulima zao hilo katika kijiji cha Lugoba Kata ya Lugoba,amefanikiwa kulima heka 5 lakini kwa kuwa hakuwa na elimu ya kilimo hicho wala hakuweza kumpata mtaalam amelazimika kutumia kilo 10 za ufuta badala ya kilo moja. “kwa kweli gharama ya kilimo hapa chalinze ipo juu ni vigumu kwa mtu wa kawaida kuimudu kwani nimelima kila heka nilitumia shilingi 70,000 kwa trekta na ufuta nikatumia sh.40,000 sawa na sh.4000 kila kilo”anasema kwa masikitiko. Felex anasema ilipofika kipindi cha kupalilia amelazimika kutenga shilingi 45,000 kila heka jambo ambalo limegarimu hela nyingi, ikilinganishwa na mkulima wa mahindi kule Dodoma ambaye anataumia shilingi 20,000 kulima heka ya mahindi. Hata hivyo felex anasema kuwa tangu aanze kulima eneo hilo hajawahi kukutana na bwana kilimo ampe ushauri namna ya kulima ufuta kwa njia bora ili aweze kunufaika. Malalamiko hayo yanaungwa na mkono na mkulima mwingine anayefahamika kwa jina la Mchungaji William yeye anasema kuwa ameishi eneo hilo siku nyingi lakini hajawahi kuwaona maafisa kilimo wakiingia mashambani kuwafundisha namna ya kulima kilimo chenye manufaa. “Hapa kwetu kumuona Afisa kilimo labda shamba limeliwa na wanyama sasa anakuja kuangalia ili atoe taarifa lakini sio kuja kutusimamia namna ya kulima hata shamba darasa hilo hawafanyi”anasema Mchungaji Wiliam. Kauli hiyo imepingwa na afisa Kilimo wa kata hiyo John Tualigo ambaye amesema kuwa wamekuwa wakifanya kazi yao lakini tatizo kubwa ni usafiri wa kutumia kuwafikia wakulima hao. “Sio kweli, tunakwenda mashambani kama mimi, nimesimamia kikundi cha wakulima katika kijiji cha Saleni tumeweza kupokea mbegu nzuri kutoka shirika la MUVI ,wakulima wamelima msimu uliopita wakavuna zaidi ya Kilo 600 za ufuta ambazo wameuza kwa shilingi 2800 kila kilo na sasa wamezitumia kulima heka 42”anasema Tualigo Anasema kuwa changamoto inayowakabili wasiwafikie wakulima kiurahisi ni usafiri kwani hata yeye alikuwa na pikipiki kama afisa Kilimo wa kata lakini ina miezi mitatu haifanyi kazi licha ya kutaalifu mwajiri wake. Tualigo anasema kuwa wakulima wa Saleni walipokea mbegu aina ya Lindi II ambazo hutoa mavuno mengi baada ya kufanyiwa utafiti na kituo cha utafiti Naliendele Mtwara. Anasema kuwa awali kikundi hicho kilikuwa na wanachama 13 lakini sasa wamefikia 32 katika msimu huu wanatarajia kuvuna zaidi ufuta ili mbegu ziuzwe katika vijiji vingine ambavyo havijapata mbegu hiyo. “Mwaka jana walikuwa wakulima 13 wakalima heka 9 wakavuna tani 2 katika msimu huu wamefanikiwa kulima heka 48 baada ya wanachama wengi kuongezeka hasa baada ya wakulimakuvutiwa na mafanikio waliyopata wale wanakindundi ambao walililipia watoto ada shuleni na wengine wakajenga”anasema Tualigo Anasema kuwa lengo la mradi huo ni kwenda kwenye vijiji vyote sita vya kata hiyo lakini njia rahisi ya kuafikia wakulima hao inashindikana baada ya kukoseka kwa nyenzo mbali mbali ikiwemo usafiri, hali inayofanaya wakulima wengi kupanda ufuta bila utaalm kwa kutupa tupa mashambani na kutumia mbegu nyingi. Naye afisa kilimo wa kijiji cha Saleni,Rashid Ali,akizumgumza katika mashamba ya ufuta yaliyolimwa na kikundi cha Saleni Seasame Farm Group, amewashauri wakulima kuungana kama walivyofanya wakulima wa kijiji hicho ambao wamefaidika kuuza ufuta kwa pamoja katika msimu uliopita,ambapo Kilo moja iliuzwa kwa sh.3000 badala ya 2000 iliyouzwa mitaani. Amewashauri wakulima kupanda mbeguza ufuta nusu inchi, chini ya udongo, inchi sita umbali wa mbegu na mbegu na futi mbili nafasi ya msitari na msitari, kabla ya kupanda wahakikishe ardhi imelainika vya kutosha na upande mbegu masaa mawili au matatu baadae. Afisa kilimo huyo amesemakuwa mbegu za Lindi 2002 zikilimwa katika eneo lililoandaliwa vizuri na kupaliliwa mapema ,mkulima anaweza kuvuna kilo 500 hadi 600 kwa heka tafauti na mbegu za kienyeji ambao mkulima huambulia kilo 100 hadi 200 kwa heka. Hata hivyo maafisa hao wanasema kuwa wakulima wakiungana na kulima zao kwa pamoja inakuwa rahisi kuhudumiwa na wataalam, wakati wakutafuta soko ni rahisi kupanga bei na takwimu za mavuno hupatikana kirahisi,hata kijiji hufaidika na ushuru wa soko. Mbegu mpya za lindi zimetajwanawakulimawengi waliozitumia msimu uliopita kwambazimeonyesha kuwavutia kutokana na ukweli kwmaba ni nyeupe na kubwa ikilinganishwa na hizi zingine za kawaida. Jasintha Wiston mkulima wa Tonga kata ya Msoga anasema “ nimeanza kutumia mbegu mpya inaitwa LINDI 2002 Eka 1 unapata gunia 8 hadi 12 tafauti na zilembegu za kienyeji ambazo huambulia kiduchu”. Wiston anasema mpaka kufikia mavuno anatarajia kuvuna kilo 300 za ufuta kwa kila heka moja na kwamba bei ya ufuta kwa kilo ni zaidi ya shilingi 2800 hivyo msimu huu anaweza kupata bei zaidi. “Katika fedha za mkopo nilizopata zilinisaidia kung’oa visiki na kulima kwa kutumia trekta la kukodisha na ndio maana nina matumaini ya kupata mavuno mengi katika msimu huu kwa sababu nimetumia kilimo cha kisasa zaidi: Kama ingekuwa ni jembe la mkono nisingeweza,” anasema mkulima huyo. Hata hivyo anaiomba serikali na wafadhili mbalimbali kutambua kuwa kilimo pekee ambacho kitamkomboa mkulima ili kuondokana na umaskini ni kilimo cha kutumia zana za kisasa na kwamba hata powertiller zinazotolewa bado hazina tija kwa mkulima kutokana na kushindwa kulima meneo yao. Mkulima mwingine anasema msimu uliopita amevuna magunia 10 ya ufuta baada ya kutumia mbegu za Naliendele, Ziada na Lindi White alizopatiwa na muungano wa vikundi vijijini muvi na kuuza gunia moja kwa Sh 240,000 na kupata Sh2.4 milioni. Mkulima huyo anatoa ombi kwa Serikali kuanzisha bodi ya zao la ufuta kama ilivyoanzisha bodi ya mazao ya pamba, kahawa na katani ili kuwainua wakulima kiuchumi wa zao la ufuta. Mafuta ya ufuta hutumika katika mapishi mbalimbali ili kuongeza ladha. Pia husaidia kuleta nguvu na joto mwilini. Mbegu za ufuta huchanganywa na vyakula mbali mbali kama mikate, keki, mboga na kadhalika. MAMBO YA KUZINGATIA WA KATI WA KUZALISHA MBEGU • Chagua aina ya mbegu inayotoa mazao mengi na bora, inayovumilia mashambulizi ya magonjwa na wadudu, inayokomaa mapema na kutoa mafuta mengi. unaweza kuchagua mbegu inayokomaa kwa pamoja ili kurahisisha uvunaji na pia kuepuka upotevu wa zao shambani. aina nyeupe ya mbegu ya ufuta hupendelewa zaidi kuliko aina nyeusi. ufuta nahitaji rutuba ya kutosha ili kutoa mazao bora. Katika kudumisha rutuba ya udongo, tumia kilimo cha mzunguko wa mazao au weka mbolea za asili pale inapobidi. kitaalamu inashauliwa kuwa mkulima adhibiti magugu kwa kupalilia ili kuruhusu ufuta kutumia vizuri unyevu na virutubishi. Magugu mengine huwa ni maficho ya wadudu waharibifu wa zao la ufuta. MAGONJWA NA WADUDU Ufuta hushambuliwa na magonjwa na wadudu mbalimbali ambao huweza kusababisha upungufu na ubora wa mazao. Hivyo kagua shamba mara kwa mara hasa kwenye maua na mapodo ili kuona dalili za mashambulizi. Endapo kuna dalili zama shambulizi, chukua tahadhari mapema kabla ya uharibifu mkubwa haujatokea. unaweza pia kukagua shamba kuona kama ufuta umekomaa. , Ufuta hukomaa, kati ya miezi mitatu na minne tangu kupanda kutegemea aina ya ufuta usiokuwa na matawi hukomaa mapema kuliko ile yenye matawi ni muhimu kuwahi kuvuna ili kuepuka ufuta kupukutikia shambani. KUKAUSHA Mapodo ya ufuta hukaushwa yakiwa yamefungwa katika vitita. Vitita huwekwa kwa kuegeshwa kwenye fremu ya kukaushia kwa muda wa wiki mbili hadi tatu kutegemea hali ya hewa. Fremu hii huwekwa juu ya turubai au sakafu ili kuzuia upotevu wa punje kutokana na kupasuka kwa mapodo.

ORA CHA PILIPILI HOHO Jina la kitalaamu la PILI PILI HOHO ni Capsicum annum. Asili ya zao hili ni bara la Amerika ya Kusini. Hapa nchini zao hili hulimwa katika mikoa ya Iringa, Tanga (Lushoto), Mbeya, Ruvuma, Tabora na Arusha. Kilimo hiki kinaendeshwa na wakulima wadogo katika maeneo yenye ukubwa wa kati ya hekta 0.2-0.4 pia kuna maeneo ya wakulima wakubwa wenye hekta kati ya 2-20. Wakulima hao hujishughulisha na kilimo cha zao hilo kwa njia ya mkataba na kampuni hiyo. Hoho hutumika katika kutengeneza rangi za asili za vyakula ambazo kwa sasa hupendwa zaidi kuliko zile zinazotokana na kemikali na pia huongeza ladha na harufu katika vyakula. Hivyo hutumika katika viwanda vya kusindika vyakula, kwa mapishi ya nyumbani na hata katika viwanda vya vipodozi kama rangi ya mdomo, uso n.k. Ina virutubisho muhimu vinavyohitajika mwilini kama madini ya chuma, vitamin A na C. 

http://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js

2.0 TABIA YA MMEA Hoho ni zao la jamii ya pilipili isiyo kali, tunda lake ni nene kiasi la duara pia linaweza kuwa lililochongoka,. 3.0 ENEO NA HALI YA HEWA INAYOFAA KWA KILIMO Hoho hustawi vema katika maeneo ya usawa wa bahari hadi mwinuko wa mita 2,000 yenye mvua ya wastani wa mm.600-1,250 na wastani wa joto la nyuzi za sentigredi 21 hadi 24. Udongo wa tifitifu wenye rutuba, usiotuamisha maji na wenye hali ya uchachu (pH) kati ya 5.0-6.5 hufaa zaidi. Umwagiliaji ni muhimu pale mvua inapokuwa chache. 4.0 UZALISHAJI 4.1 UTAYARISHAJI WA KITALU Chagua eneo katika ardhi isiyo na mtelemko mkali na yenye rutuba ya kutosha. Ardhi iwe imepumzishwa bila kuoteshwa mazao ya jamii ya pilipili, biringanya, nyanya, n.k. ili kuepukana na mashambulizi ya wadudu na magonjwa. Tayarisha kitalu kabla ya msimu wa mvua. Andaa vizuri matuta manne yenye urefu wa wastani wa mita 10 kila moja na upana wa mita moja (1) ili kustawisha miche inayotosha ekari moja. Acha njia ya nusu mita kati ya tuta na tuta. Mwagilia maji ya kutosha siku moja kabla ya kusia mbegu na endelea kunyweshea kulingana na hali ya hewa na hali ya udongo. Sia mbegu kwenye, mstari, nafasi kati ya mstari na mstari ni sm 10 na kina cha sm1. Kiasi cha mbegu cha nusu kilo kinatosha eneo la hekta moja. Weka matandazo kwenye kitalu au tumia nailoni nyeusi ili kuhifadhi unyevunyevu na kuzuia uotaji wa magugu. 4.2 UTAYARISHAJI WA SHAMBA Shamba lilimwe vizuri na kuweka matuta ili kuhifadhi unyevunyevu na kurahisisha umwagiliaji. Matuta yanaweza kuwa makubwa au madogo kulingana na matakwa ya mkulima. Matuta makubwa hupandwa mistari miwili na matuta madogo hupandwa mstari mmoja.  4.3 UPATIKANAJI WA MBEGU Mbegu ambazo hutumika ni chotara ambazo huuzwa kwenye maduka ya pembejeo za kilimo nchi nzima. Haishauriwi kutumia mbegu kutoka zao la msimu uliopita kwani ubora wa paprika utaharibika na hivyo kuharibu soko unashauriwa kununua mbegu bora. 4.4 UPANDAJI Mbegu huoteshwa na kukuzwa kitaluni kwa muda wa wiki 6-8 na miche hupandikizwa shambani ikiwa na urefu wa sm.6-10. Mwagilia maji kitaluni kabla ya kuhamisha miche. Panda shambani kwa nafasi ya sm.75-90 kati ya miche kwa sm.90-105 kati ya mistari, wastani wa miche 12,500 itapatikana kwa hekta. Weka samadi shambani tani 25-37 kwa hekta wiki 1-2 kabla ya kupandikiza miche, au kilo 560-670 za NPK (mbolea ya viwandani) kwa hekta kwa uwiano wa 4:7:7 katika udongo usio na rutuba ya kutosha. ITALIAN PAPRIKA  5.0 KUHUDUMIA SHAMBA Palizi ifanyike mara magugu yanapotokea shambani. Umwagiliaji maji ufanyike kama ilivyo kwa mazao mengine kama nyanya. Tumia mbolea kiasi cha kilo 140 za SA au CAN kwa hekta hasa wakati mmea inapotoa matunda ili kupata matunda makubwa na kuvuna kwa muda mrefu (hadi miezi 10). 6.0 MAGONJWA NA WADUDU Wadudu • Funza wa vitumba • Vidukari • Kidomozi (Leaf miner) Kudhibiti: Tumia dawa aina ya permethrin Magonjwa • Kuoza mizizi • Mnyauko wa majani • Batobato Kudhibiti: Choma nyasi kwenye kitalu kabla ya kusia mbegu. Badilisha mazao yasiyo ya jamii ya pilipili. 7.0 UVUNAJI Matunda ya kwanza huwa tayari kuvunwa kuanzia miezi 2-3 baada ya kupandikizwa; matunda yaliyokomaa vizuri na kuwa na rangi nyekundu ndiyo huvunwa. Matunda 30-80 hupatikana kwa mmea mmoja. Ubora wa hoho huongezeka kutegemeana na kiwango cha rangi yake ikiwa ni nyekundu njano au kijani. Mazao kiasi cha tani 3.5 kwa hekta hupatikana. Baada ya kuvuna mwagilia maji, piga dawa (kama ni muhimu) na weka mbolea kuongeza uzalishaji unaofuata. 8.0 USINDIKAJI Hoho huuzwa ikiwa bado fresh tofauti na jamii nyingine za pilipili ambazo zinaweza kukaushwa na kusindikwa kasha kuuzwa baadae.  9.0 SOKO LA PAPRIKA Soko la hoho lipo nchi nzima kwenya masoko makubwa na hata magengeni, hoho hutumiwa zaidi kama kiungo cha kupikia mapishi mbali mbali au kutia kwenye kachumbari. Tatizo kubwa wanalokabiliana nalo wakulima ni kutokuwa na soko la uhakika ndani na nje ya nchi, mazao huweza kuoza shambani au njiani kutokana na tabu ya usafiri hasa vijijini ambapo mvua zikinyesha barabara hazipitiki kwa urahisi Kuna aina ya pilipili isiyo kali kama hoho lakini ni ndefu kama pilipili za kawaida ijulikanayo kama PAPRIKA ambayo ina soko kubwa nje ya nchi. Zao hili kwa sasa huzalishwa kwa msukumo wa kampuni ya kigeni ya Hispania inayoitwa Tanzania Spices Ltd iliyopo mkoani Iringa  10.0 GHARAMA YA UZALISHAJI WA HEKTA MOJA: Mbegu Tshs. 24,000 /- Vibarua 200,000/- Mbolea(mboji/samadi) 300,000/- Madawa 100,000/- Jumla 624,000/- MAPATO: Kilo 3,500/- X 800/- 2,800,000/-

KILIMO cha tangawizi katika Wilaya ya Madaba kinaanza kusambaa kwa kasi kutokana na juhudi za Mbunge wa jimbo hilo, Joseph Mhagama kwa uamuzi wake kuwainua wananchi kiuchumi. Kiongozi huyo amehamasisha kilimo hicho na kugawa tani sita za mbegu ili wananchi waweze kunufaika kwa kuwa zao hilo limepata soko nchini Kenya.

http://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js
Anasema, ni jukumu la viongozi kuhimiza wananchi walime mazao yanayoonesha kuwainua wananchi kiuchumi yakiwemo ya tangawizi, mbaazi, alizeti na maharage. Mhagama anasema, kilimo cha tangawizi kimewezesha wakulima 2,745 kubadili maisha na wapo waliojenga nyumba bora na wengine wamenunua vyombo vya usafiri yakiwemo magari, pikipiki na baiskeli. Anasema, kila siku wafanyabiashara Kenya wanahitaji tani 50 za unga wa tangawizi hivyo ni lazima wananchi wa jimbo hilo wakipende kilimo hicho ili kiweze kuwainua kiuchumi na kufanikisha ustawi wa jamii. “Nimefanya utafiti na kubaini kuwa zao hilo litawaondoa wapigakura wangu kwenye lindi la umasikini,”anasema Mhagama. “Kabla sijawa Mbunge wa Jimbo la Madaba mwaka 2012-2014 nikiwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilokuwa la kiserikali Ruvuma Commercialization and Diversification of Agriculture (RUCODIA) nilifanya utafiti kuhusu shughuli za kilimo na mifugo juu ya mazao yenye tija zaidi, baada ya kubaini umasikini wa kipato unaowakabili wakulima wadogo umekuwa ukichangiwa na kilimo kisichokuwa na tija kwa wakulima mkoani hapa,”anasema. Baada ya kugundua hilo shirika hilo limeelekeza nguvu kwenye mazao ya alizeti na tangawizi kwa kuwa linaamini kwamba linaweza kuinua maisha ya wakulima wadogo na kuwaongezea kipato zaidi badala ya kuendelea kulima kilimo kisichokuwa na tija. Limeunda vikundi vya wakulima wadogo na kuwahamasisha kwa kuwaahidi soko la uhakika la kuuzia mazao yao, kabla ya kupeleka kiwandani kwa kazi ya usindikaji na kuzalisha mafuta ya alizeti yenye ubora. Anasema shirika lilianza na wanachama wakulima 300, lakini mpaka sasa wamefikia wakulima 2,745. Mbegu zilizopandwa wakati huo zilikuwa kilo 10 lakini sasa kuna tani 9,000 hivyo kuonesha kuwa wananchi wamehamasika kujikomboa kiuchumi. Mhagama anasema, wananchi wanatakiwa wazalishe kwa wingi mazao muhimu kwa kiuchumi kwa wilaya ya Madaba. RUCODIA ina jukumu la kuhakikisha mazao ya wakulima yananunuliwa. Shirika hilo limenunua tani zaidi ya 850 za alizeti kwa bei ya Sh 450 kwa kilo moja na kuwawezesha kuwalipa zaidi ya Sh 502,500,000. Wameweza pia kununua tani zaidi ya 600 za tangawizi kwa bei ya Sh 1,000 kwa kilo na wameweza kuwalipa wakulima wa zao hilo zaidi ya Sh milioni 500. Mratibu wa Rucodia, Ladislaus Bigambo anasema, tangawizi ni kiungo ambacho sehemu inayotumika ni tunguu (rhizome) ambayo huonekana kama mizizi ya mmea. Anasema, asili ya zao hilo ni maeneo ya kitropiki ya bara la Asia na hasa katika nchi za India na China. Bigambo anasema zao hilo linazalishwa kwa wingi kutoka katika nchi ya Jamaica na kwa hapa nchini zao hili hulimwa katika mikoa ya Ruvuma Wilaya ya Madaba, Kigoma, Tanga, Morogoro, Pwani, Mbeya na Kilimanjaro. Anasema tangawizi hutumika kuongeza ladha, harufu na kuchangamsha katika vinywaji ikiwemo chai, soda, juisi, vilevi na vyakula mbalimbali kama vile mikate, biskuti, keki, nyama za kusaga, na achari. Bigambo anasema, zao hilo hutumika pia katika viwanda vinavyotengeneza dawa ya tiba ikiwemo ya meno, kikohozi, tumbo na muwasho wa ngozi wakati mwingine pia hutumika katika vipodozi kama poda. Zao hilo hustawi katika maeneo yenye hali ya kitropiki, kutoka usawa wa bahari hadi mwinuko wa mita 1,500 au zaidi na huhitaji mvua kiasi cha mm. 1,200-1,800 na joto la wastani wa nyuzi za sentigredi 20-25 na hustawi vema katika udongo tifutifu wenye rutuba na usiotuamisha maji. Mkulima wa zao hilo kutoka Mkongotema, Menas Mgaya anasema, elimu inayotolewa na RUCODIA imewawezesha kupiga hatua za kimaendeleo kwa kulima mazao yenye tija na yenye uhakika wa soko kwani wamefanikiwa kufanya hivyo baada ya kuwahamasisha na kuitikia mwito wao na kuunda kikundi chao ambapo kupitia kikundi hicho wamekuwa wakiuza mazao yao na kujipatia fedha Mgaya anasema, kupitia kilimo hicho sasa wana uhakika wa chakula na watu wanazimudu gharama za huduma muhimu kama elimu ya watoto, afya na makazi bora. Kwa mujibu wa mkulima huyo, awali walikuwa wanashindwa kuzitumia vyema maliasili kama misitu , ardhi, maji na hali ya hewa iliyopo wilayani mwao hivyo watu wengi wakashindwa kuwa na sauti katika jamii au kushiriki katika mipango, ufuatiliaji na uamuzi na kubaki wanyonge kutokana na umasikini. “Laiti kama tungalitumia mbinu za kijasiriamali, au kilimo chenye manufaa tungekuwa mbali sana kiuchumi,”anasema Mgaya. “Tungekuwa na uwezo mkubwa zaidi wa kumudu maisha, tena kwa kujiamini kuliko ilivyo sasa kama kweli viongozi wetu wangekuwa wanatumia utafiti sahihi wa kuondokana na umasikini katika maeneo yetu kuliko kuendelea kufanya maisha ya kilimo au kiujasiriamali bila utafiti,”anasema. Mkulima kutoka Magingo, Osmund Njelekela anasema, zao la tangawizi ni mkombozi kwa wakulima wa eneo hilo kwa kuwa limewaondoa kwenye unyonge na umasikini. Njelekela anasema, siku za mwanzo hali ya umasikini kwenye kaya zao ilikuwa imekithiri na kuwafanya hali hiyo kuwakosesha elimu na huduma nyingine kwa watoto na wakashindwa kumudu kuzihudumia familia. Wakulima wameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kudhamiria kuinua uchumi wa mtu wa kati kwa kutoa mbegu za tangawizi na vitendea kazi. Wanasema kukiwepo rasilimali ardhi, na watu wakipewa nyenzo Tanzania haitakuwa miongoni mwa nchi zinazolalamika na umasikini kwa kuwa mito ipo, maziwa yapo pamoja na mvua za kutosha. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Madaba, Vastus Mfikwa anasema, kwa kushirikiana na Mbunge wameweza kuzitembelea kata zote na kuainisha vipaumbele vya kuwakomboa wananchi kiuchumi kielimu na kiafya. Mfikwa anasema Mbunge ametoa mbegu tani sita za tangawizi, ameweza kugawa pikipiki 3 pamoja na baiskeli 6 kwa ajili ya walemavu na baiskeli nyingine kupeleka katika kituo cha afya Madaba ili iweze kusaidia wagonjwa wasiojiweza kutembea kutoka wodi moja hadi nyingine. Anasema, kwa muda mrefu Mbunge Mhagama amekuwa akishirikiana zaidi na wananchi kwa kuanzisha miradi kwa wakulima wadogo ikiwa ni pamoja na kilimo cha ufuta, alizeti na tangawizi hivyo ameahidi kushirikiana na madiwani wenzake kuhakikisha jimbo hilo linakua kwa kasi kiuchumi. Kwa mujibu wa Mfikwa, Halmashauri ya Madaba ina jimbo jipya na ina wananchi wenye vipato vidogo hivyo wanahitaji kujengewa uwezo zaidi ambao utamwezesha kila mwananchi ambaye ni mkulima kuwa na kipato kisichopungua Sh 300,000 kwa mwezi. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Madaba, Robeti Mageni amewataka wadau wa maendeleo kujitokeza kwa wingi ili waweze kushirikiana kuipaisha kiuchumi wilaya hiyo. Anatoa changamoto kwa wazawa wa eneo hilo ambalo wapo ndani na nje kutumia fursa za kiuchumi zilizopo wilayani humo na wajitahidi kila moja kwa nafasi yake kuwezesha maisha yenye

Ndugu zangu, wiki iliyopita nilihamsika sana baada ya baadhi ya wasomaji kuniandikia barua pepe na wengine kunipigia simu kutaka ufafanuzi kuhusu kilimo cha Maembe, na kilimo cha miti na organic farming kwa ujumla, kilimo ambacho nilianza nacho miaka mitatu iliyopita nikitokea shuleni. Mwaka uliopita niliandika makala kuhusu wasomi kujifunza kujiajiri nilikusudia kuwasilisha ujumbe mmoja ya kwamba, "Wasomi" na Watanzania kwa ujumla wetu tunatakiwa kubadilisha mitazamo yetu ili kujipatia mipenyo ya kiuchumi na kifedha (financial freedom). Kimsingi ni kwamba zipo imani zinazosapoti watu kuwa na fedha za kutosha na zipo imani na mitazamo inayozuia watu kuwa na fedha ama inawafanya waishi maisha ya kupungukiwa nyakati zote! Imani na mitazamo hii kimsingi huzalishwa kutokana na malezi, utamaduni na mazingira. Mtazamo wa mtu kuhusu fedha tunaita, “Money blue print.” Nafahamu kuwa wengi kama sio wote tunakubaliana kuwa fedha zina umuhimu mkubwa sana katika maisha ya mtu, na kwamba ukosefu wa fedha ndio msingi wa maovu(Ingawa wapo watu wanatumia fedha kufanya uovu wao) tunachotofautiana ni imani kuhusu fedha. Mitazamo kuhusu fedha ndio inayoamua kiwango cha fedha alichonacho kila mmoja. Hii ina maana kuwa kila mtu anamiliki kiwango cha pesa sawa sawa na imani ama mtazamo wake kuhusu fedha. Miaka michache iliyopita wakulima walikuwa ni watu wanaotazamwa kama watu wenye shida, walio jitokeza kuwekeza kwenye kilimo walionekana wameshindwa shule (waliokimbia umande). Na hii ilisababishwa na imani ama mapokeo ya tuliyorishwa na wazazi wetu na walimu wetu kutoka kwenye kipindi cha zama za viwanda (Industria Age). Lakini kwa sasa dunia imebadilika sana, kilimo kimewafikisha watu kwenye ndoto zao, Nimesoma kwenye jarida la Forbes kwamba tajiri wa kwanza Afrika amewekeza kwenye kilimo, wajarisiamali wakubwa hapa Tanzania wamewekeza kwenye kilimo, na wale wanaojiona wameenda shule ‘middle class’ wanaendelea kushangaa na kuendelea kuongea sentensi hasi na kulalamikia viwango vidogo vya mishahara. (Kazi kweli kweli.) Miaka ya hivi karibuni kwenye Mikoa ya Arusha, Manyara, Iringa, Mbeya,Tanga, Singida na Kilimanjaro zao la vitunguu limejizolea umaarufu mkubwa kwa kuendelea kuajiri maelfu ya Watanzania. Kuna ambao wamefikia ndoto zao kupitia kilomo cha vitunguu, wamejenga nyumba, wamefungua makampuni yao, wanasomesha watoto nk. Vitunguu hivi hivi kuna rafiki zangu wamenunua magari ya ndoto zao, wamejipa likizo nchi za nje. Nitaongelea hasa eneo la Ruaha Mbuyuni na Mahenge sehemu ninayolima mimi. Hali ya hewa na maji ni vipengele muhimu sana vya kuzingatia katika uzalishaji wa zao la vitunguu.Vitunguu vinastawi vizuri katika hali ya ukavu kwa kutumia umwagiliaji.(Local Irrigation) Maji mengi hasa wakati wa masika husababisha magonjwa mengi hasa ukungu, vitunguu haviwezi kukomaa vizuri, hivyo kusababisha upotevu mkubwa wa mazao. Aina ya mbegu tunayolima sisi pale Mahenge na Ruaha Mbuyuni ni pamoja na Mang’ola (traditional) red, Red creole na Bombay Red. Hizi ni mbegu bora ambazo zinatoa mazao mengi kuanzia magunia 70- 90 kwa hekta ikiwa kilimo bora kitazingatiwa na iwapo mkulima atakuwa anaongozwa na malengo yake na hamasa ya ndani (self drive) Mkulima anaweza kuchagua mbegu kwa kuzingatia, soko, msimu wa kupanda nk. Wasambazaji wa mbegu ni pamoja na maduka ya TFA, na maduka ya bembejeo za kilimo katika maduka mbalimbali. Ingawa wapo baadhi ya watu hasa maeneo ya Ilula –Iringa ambao huandaa wenyewe mbegu kwa kutumia maua ya vingunguu. Uandaaji wa kitalu hutegemea sehemu husika, lakini kwa kifupi Sehemu ya kitalu iwe wazi, mbali na kivuli na kiwe karibu na chanzo cha maji na huchukua takribani wiki tano mpaka sita kabla ya kupelekwa kwenye shamba husika. Zipo changamoto mbalimbali ambazo hujitokeza kwenye maandalizi ya kitalu mpaka shambani, changamoto hizo ni pamoja na wadudu, ugonjwa wa ukungu, Wadudu waharibifu ni pamoja na Chawa wekundu ambao wanashambulia majani, na wadudu waitwao Sota ambao hukata miche. Ili kudhibiti tatizo, shamba likaguliwe mara kwa mara kuona dalili za mashambulizi. Endapo kuna dalili za mashambulizi, mkulima – mjasirimali ana shauriwa kuchukua hatua za kuzuia kabla uharibifu mkubwa haujatokea ambao husabaisha wakulima wapya kukata tama na kurudi kule kule kwenye kuilamikia serikali kwamba haiwajali. Baada ya maandalizi ya kitalu na mbengu kupelekwa shambani, hatua inayofatia ni ufatiliaji wa malakwamala kwa kupulizia dawa na palizi. Iwapo mkulima yupo mbali na eneo husika, kwa mfano yupo Mwanza, Dar, Moshi ama popote Duniani, mkulima atalazimika kuajiri vijana ambao watamfanyia kazi kwa malipo mpaka vitunguu vitakapo komaa. Miche ya vitunguu, huota taratibu sana, hivyo miezi ya mwanzoni, miche husongwa sana na magugu. Palizi mbili mpaka tatu zinashauriwa na zinatosha kuweka shamba safi. Kabla ya kuanza kuvuna vitunguu mkulima anashauriwa kukagua shamba ili kuhakikisha kuwa vitunguu vimekomaa. Na iwapo upo mbali na shamba lako hakikisha unatembelea shamba lako malakwamala. Dalili ya vitunguu kukomaa ni, majani kunyauka na kuanza kukauka asilimia 80 -100% na majani kukauka. Mpaka sasa hapa Tanzania, vitunguu huvunwa kwa mikono. Mimea inangolewa au kuchimbuliwa kwa kutumia jembe dogo. Baada ya kuvuna vitunguu vinaweza kuachwa shambani vikiwa vimefunikwa na majani kukinga jua kwa muda wa siku mbili au tatu kutegemeana na hali ya hewa. Lengo nikuimarisha ngozi(Nyama) ya vitunguu nk. Pia kupunguza unyevu kwenye majani na mashina na kuruhusu sehemu ya chini ya shingo kufunga. Ikiwa usalama ni mdogo, vitunguu vinachambuliwa na kukatwa majani na mizizi na kuanikwa sehemu nyingine. Ukaushaji hutumia wiki mbili kutegemea hali ya eneo. Kwa sasa soko la vitunguu lipo juu sana,Watu wa kada mabalimabali wanahusika na ununuzi na uuzaji wa vitunguu wakiwa ni pamoja na: wakulima, wachuuzi, wafanya biashara ndogondogo, wauza jumla, wauza rejareja, wasafirishaji na madalali. Kutoka shambani mpaka sokoni. Kama nilivyotangulia kusema hapo juu, hekari moja inaweza kutoa magunia 80-100 kwa sasa maeneo ya Njombe, Iringa, na Kwingineko gunia moja la vitunguu huuzwa kati ya shilingi 130,000/= mpaka laki 150,000/= lakini mkoani Njombe kwa bei ya sasa gunia moja ni shilingi 200,000/= kwa gunia. Ingawa kuna baadhi ya misimu soko hushuka sana mpaka kufikia shilingi laki moja kwa gunia ama elfu 70.(Kumbuka kwamba kutafuta pesa ni sawa na mchezo wa mpira wa miguu kadiri unavyo ucheza ndiyo unavyo kuwa hodari-uchaguzi ni wako) Ukiwa na gunia labda 70 ukaziuza unaweza pata hadi shilingi milioni milioni 9, kwa ekari moja baada ya kuondoa gharama yote. Sasa ukiwa na ekari 5, 6,ama 3 utakuwa na shilingi ngapi? Wakati huo unasubiri mshahara wako. Kaka yangu mimi kwa msimu uliopita alipata magunia 1000, ni utajiri gani huu? Kila mtu anayo nafasi sawa (equal channce) ya kuwa na fedha za kutosha kumpa uhuru wa kiuchumi. Pili hakuna raha wala sifa ya kuendelea kuwa masikini, kama unafikiri nisifa ama unajidanganya kuwa masikini watapunguziwa adhabu siku ya mwisho unapoteza muda wako kwa sababu masikini ni mzigo kwa dunia. Masikini na umasikini wake hata awe ni mtakatifu na mwema kiasi gani ni kwamba anaitesa dunia (kwa sababu anahitaji kusaidiwa). Tajiri (ama niseme mwenye fedha za kutosha) hata kama ni mchoyo ama bahiri bado ni msaada kwa dunia (kwa sababu anajisaidia). Ninatamani kila mmoja apokee changamoto ya kutamani kuwa na uhuru wa kifedha na kiuchumi kwa kuanza na vitu tunavyo viona ni vidogo kwenye macho yetu ama kuachana na kasumba tuliyopewa shuleni kwamba ukimaliza kusoma lazima usake ajira. Ajira zenyewe hakuna na zilizopo bado ni chache. Na hili linawezekana ikiwa mitazamo na imani za wengi kuhusu fedha zitabadilika na kuwa zinazosapoti badala ya kuvuruga nafasi ya mtu kupata fedha. Kila Mtanzania anastahili ushindi wa kifedha. Wengi wetu tumekuwa watu wa kuhangaikia malengo ya wenzetu, kuna watanzania wenzetu wapo tayari kuzungumzia Malengo za timu za ulaya siku nzima, wiki, mwezi na jinsi ya kuhakikisha wanapata ushindi n.k., mtu huyohuyo hana ajira, ama aliyonayo mshahara hautoshi. Kwa watanzania watakao penda kufanya kilimo hiki ama kile cha miti wanaweza kunitafuta nikawapa maelezo ya kutosha. Nchi hii ina matatizo mawili ya msingi kwenye kipengele cha Ujasiriamali, kuna wanaozifahamu fursa lakini hataki kuziweka wazi, sijuwi wanaogopa nini? Labda wana hofu ama ni wachoyo. Pia, kuna wale ambao walishazisikia fursa lakini bado wanasema nitaanza kesho na wapo wale wanaosingizia mitaji, umbali n.k.

Kambale (Ietalurus Punetaus), ni aiana ya samaki ambao wana majina mengi kulingana na eneo na jamii husika. Samaki hawa unaweza kusikia wakitajwa kwa majina mengine kama vile, kambale channel, koleo, samaki kidevu n.k. Asili ya Kambale Asili ya samaki hawa ni Amerika ya Kaskazini. Samaki hawa hukua kwa haraka sana, na kuwa na uzito mkubwa. Aina hii ya samaki hupendwa na watu wengi kwa kuwa nyama yake ina ladha nzuri na ni laini sana. Samaki hawa huzaliana vizuri zaidi wanapokuwa mtoni au sehemu ambayo wanapata tope. Mfugaji anapokusudia kufuga aina hii ya samaki kibiashara, ni lazima kusakafia bwawa ili kuepuka uharibifu unaoweza kusababishwa na samaki hawa. Umbile lake Samaki aina ya kambale wana umbo refu, mpana kuanzia shingoni, ingawa kichwa ni kidogo, na upande wa mkia ni mwembamba. Samaki hawa wana rangi ya kijivu na wengine nyeusi. Jinsi ya kulisha kambale Unaweza kulisha kambale kwa kutumia unga wa samaki, maharagwe yaliyosagwa, mahindi, mchele pumba, ngano na bidhaa nyingine. Unaweza kujenga mfumo ambao utawawezesha samaki hawa kupata aina mbalimbali za wadudu, pamoja na majani, ili kusaidia wapate mlo kamili. Ukuaji na uvunaji wa kambale Aina hii ya samaki, wakitunzwa vizuri, wanaweza kukua kwa haraka na kuwa na uzito mzuri unaoweza kumpatia mfugaji faida nzuri. Unaweza kuanza kuvuna kambale baada ya miezi sita tangu walipopandikizwa kwenye bwawa. Soko la kambale Fikiria soko la samaki kabla ya kuanza kuzalisha. Wafugaji walio wengi, wamekuwa wakianzisha miradi ya ufugaji wa samaki kwa kufuata mkumbo bila kutambua kwanza soko watakalozalishia samaki hao. Jambo hili huwafanya wafugaji kuwa na kipato kidogo tofauti na nguvu waliyotumia kuzalisha. Inapofikia wakati wa kuvuna samaki, kiasi kikubwa huuzwa papo hapo bila kufika kwenye soko halisi, jambo linalosababisha kipato kuwa duni. Ni vyema mfugaji akawa na soko maalumu ambalo atazalishia. Unaweza kuzalisha kwa ajili ya shule, hospitali, vyuo, au taasisi yoyote. Halikadhalika jamii inayokuzunguka na taasisi nyinginezo. Mambo ya kuzingatia kabla ya kufuga samaki • Fahamu ni aina gani ya samaki inayopendwa zaidi katika eneo ulipo. • Samaki wanaopendwa wanatakiwa wawe na ukubwa gani. • Kiasi cha samaki kinachohitajika katika soko ulipo. • Ni kipindi gani ni kizuri kwa uvunaji wa samaki. • Ni wakati gani mzuri wa kuuza samaki. • Je, katika eneo lako kuna mfugaji mwingine anaezalisha samaki kwa ajili ya soko hilo?. • Bei ya aina ya samaki unaozalisha ikoje? Wasikilize wateja Wakati wote mfugaji anapouza samaki, ni lazima kusikiliza kwa umakini, wateja wako wanasemaje. • Je, wanapendelea samaki unaouza. • Je, samaki wako ni wadogo sana au ni wakubwa sana. • Wakija kununua wananunua kwa kiasi gani, kikubwa au kidogo. • Je, wanapendelea uzalishe zaidi? • Je, kuna wafanyabiashara wanataka uzalishe zaidi ili nao wanunue. • Wanataka samaki wawe kwenye ubora gani. • Wanaridhika na bei unayowauzia. Fuata haya kwa ufanisi wa soko la samaki • Hakikisha samaki wako katika hali ya usafi na vyombo salama unapovua tayari kwa kupeleka sokoni. • Samaki ni bidhaa inayoharibika kwa haraka, hivyo hakikisha unawapeleka sokoni mara tu baada ya kuwavua. • Hakikisha gharama za usafiri, utunzaji na uhifadhi, zinalipwa kutokana na bei ya soko. • Kumbuka gharama za uhifadhi wa bidhaa inayoharibika haraka kama samaki ni kubwa, hivyo vua kwa awamu kulingana na mahitaji. • Unaweza kuongeza thamani ya samaki kwa kufanya mambo ya msingi yanayohitajika kwenye uandaaji wa samaki, kama vile kuparua na kutumbua. • Unaweza kuwasafisha, na pia kuwakaanga kulingana na soko husika. Kwa kuzingatia mambo hayo machache, mfugaji anaweza kufanya maamuzi sahihi kabla ya kuwekeza kwenye mradi wa ufugaji wa samaki. Pia ni muhimu kuzingatia mahitaji muhimu ya ufugaji wa samaki, ili kuepuka gharama zisizo za lazima. Tengeneza chakula cha samaki mwenyewe Mfugaji anaweza kupunguza gaharama za kununua chakula kwa ajili ya samaki, kwa kutengeneza chakula mwenyewe kwa kutumia malighafi ulizo nazo katika eneo lako. Tumia resheni rahisi ambayo itakupatia chakula cha kutosha na kwa gharama nafuu. Mahitaji • Pumba ya mahindi sadolini 1. • Pumba ya ngano au mpunga sadolini 1. • Dagaa sadolini 1. • Kilo moja ya soya. • Robo kilo ya mashudu ya pamba au alizeti. Namna ya kuandaa • Changanya malighafi hizo kwa pamoja. • Saga hadi zilainike. • Kanda kama vile unga wa kutengenezea chapati. • Weka kwenye mashine ya kusaga nyama au kutengenezea tambi. • Anika kwenye jua la wastani. • Baada ya kukauka, vunja vunja kwenye vipande vidogo vidogo hasa kwa kuzingatia umri wa samaki unaokusudia kuwalisha. • Tumia lishe hiyo kwa samaki mara tatu kwa siku.

Kilimo cha Tikiti Maji TIKITI, UDONGO NA JOTO Usiwe wa kutuamisha maji Ukiwa Tifutifu, AU kichanga Tifutifu (Clay loam) na hali ya joto kiasi angalau 15- 35 degree inatosha sana Linahitaji maji mengi mwanzoni lakini kadri linavyoendelea maji unapaswa kupunguza MUDA WA KUOTA Ukisia mbegu huchukua siku 5 hadi 10 kuota KAMA SHAMBA LIKO TAYARI BY NOW, UKIPANDA SIKU 75 HADI 90 (AINA ZA MBEGU ZILIZOPO SOKONI KWA SASA NI HYBRID -ZEBRA, 1. SUKARI F1, 2. MSHINDI, 3. JULIANA ETC) UNAVUNA TIKITI KWA HIYO UNAMIEZI 3, OKT, NOV NA DEC WAKATI TUNAKABIA MWAKA MPYA UNAVUNA. KWA TIKITI JITAHIDI SANA KUPANDA KWA NAFASI KAMA UTALIMA MATUTA BASI TUTA LIWE LIMEINUKA KIASI KUJA JUU WALAU SM 20 HIVI LIWE NA UPANA WALAU WA SM 45 HADI 60, UPANDAJI, KUTOKA SHIMO HADI SHIMO SM 90 HADI 100, NA KUTOKA KATIKATI YA TUTA HADI TUTA LINGINE NI MITA 1.5=SM 150, KWA HIYO KWA MATUTA YANAYOFUATANA TIKITI ZIIKIANZA KUTAMBAAA UNAZILAZA ZINAKUTANA KATIKATI YA HIZO TUTA MBILI KAMA UTAAMUA KUPANDA KWA MAJARUBA KAMA HAYA YA MPUNGA, AMBAPO WATU WENGI HUMWAGIA KWA KUTENGENEZA MITALO YA KIENYEJI YA UMWAGILIAJI BASI, JARUBA LAKO LINAPASWA KUWA NA UPANA WA MITA 3 NA UREFU WOWOTE ULE HATA WA MITA 5 ILI MRADI UWEZE KUMUDU KUINGIZA MAJI. SASA KWA JARUBA TUNAPANDA PEMBENI KATIKA ANGLE HIZO. KUTOKA SHIMO HADI SHIMO NI HIZO SM 90 (=futi tatu), AMBAPO SASA YAKIAANZA KUTAMBAA UTAYALAZIA KATIKATI HAPO KATIKA HUO UPANA WA MITA 3, SO YA KULIA YATAKUJA HAPO CENTRE, YA KUSHOTO , KASK, NA KUSINI HIVYO HIVYO YANAKUJA KULALA HAPO MBOLEA ZA KUPANDIA NI MUHIMU SANA UKIPATA YARA MILA WINNER ( NAMBA HIZI 15:9;20 AINA YA NPK) ITAKUFAA KILA SHIMO UNALOWEKA MBEGU MOJA WEKA GRAMA 10 YA MBOLEA SWA NA KIJIKO KIMOJA KIKUBWA CHA WALI. ZITAOTA BADA YA SIKU 5 HADI 10 AFTER ONE-THREE WEEKS TANGU KUOTA MBEGU, UTAWEKA MBOLEA YA KUKUZIA KAMA CAN AU UREA (UREA UIWEKE BAADA YA KUWA UMEMWAGIA MAJI MENGI SHAMBANI) MAUA YAKIJA JITAHIDI UPATE BOOSTER (HIZO NI MAALUMU KWA AJIRI YA MAUA NA MATUNDA ZIPO BOOSTER ZINAITWA STAARTER- MFANO HALISI ZILIZOPO MADUKANI NI POLYFEED STARTER-HIZO HUTUMIKA KUPIGA MAUA WAKATI WA MAUA MATUNDA YAKIJA UTAWEKA POLYFEED FINISHER-HIYO NI KUIMARAISHA MATUNDA, NA PIA UTAFUTE MBOLEA INAITWA YARA NITRABOR (HII INA Calcium na Nitrojen kwa wingi) , husaidia kuzuia tikiti kunyauka, na kuzoa katika kitako-Ugonjwa unaitwa Blosom End Rot WAKATI WOOTE WA MAISHA YA TIKITI USISAHAU DAWA ZA WADUDU, WANAOKATA MAUA , NA KUTOBOA MATUNDA, DAWA KAMA DUDU ALL AU SELECRON, AU MATCH, AU KARATE MOJA WAPO YATOSHA KUMALIZA WADUDU LAKINI WAKATI WA KUPIGA HIZI DAWA KUWA MAKINI SANA USIPIGE MCHANA, UTAUWA NYUKI WA KUFANYA UCHAVUSHAJI KUTOFANYIKA-HAPO UTAPATA DIFORMALITIES NYINGI SANA KAMA SHAPELESS KATIKA MATUNDA, PIGA ASUBUHI SANA AU JIONI SANAA, PIA KAMA UTAONA KUNA HALI YA UKUNGU (UNYEVU NI MWINGI AU BARIDI USIKU AU MCHANA) NI MUHIMU KUWEKA DAWA ZA JAMII YA COPPER, KAMA BLUEE COPPER, AU EBONY KUZUIA UKUNGU, NI MUHIMU SANA KUHAKIKISHA TIKITIKI ZAKO ZINAPATA MAJI WALAU MARA 3 KWA WIKI, ILI KUPUNGUZA WATER SRESS GHARAMA ZA MBEGU KWA EKARI MOJA UTAHITAJI Gram 300 za mbegu , ambapo jumla ya gharama za mbegu ni kati ya tsh 200,000 hadi tsh 300,000 MAVUNO Kwa kuwa kwa nafasi tajwa hapo juu utakuwa na mashimo yasiyopungua katiya 2000 hadi 3000 Kwa ekari moja. Hivyo kila shimo au kila kamba ya tikiti ikikupa matikiti matatu means utakuwa na mavuno ya vichwa vya tikititi kati ya 6000 hadi 9000, ambayo ni sawa na wastani wa tani 12 hadi 18 kwa ekari moja