Sports
Tafadhali Share na marafiki story hiiSports
Tafadhali Share na marafiki story hiiSports
Tafadhali Share na marafiki story hiiLiverpool imeanza kumwinda mshambuliaji wa Southampton Sadio Mane katika uhamisho wa kitita cha pauni milioni 30. Mkufunzi wa klabu hiyo Jurgen Klopp anamtaka mchezaji huyo wa miaka 24 kutoka Senegal kuimarisha safu ya mashambulizi na anapanga kuufanya uhamisho wake kuwa wa kihistoria katika kilabu hiyo. Liverpool na Southampton zitaendelea kufanya mazungumzo kuhusu mpango huo huku kitita hicho cha uhamisho kikiwa swala muhimu. Southampton wanadaiwa kutaka pauni milioni 40 kwa mchezaji huyo ambaye alifunga mabao 11 katika mechi 37 alizocheza msimu uliopita. Kitita hicho ni pauni milioni 10 zaidi ya kile kinachopendekezwa kutolewa na Liverpool swala ambalo litahitaji mazungumzo zaidi kabla ya mpango huo kuidhinishwa. Image copyrightAP Image caption Jurgen Klopp Southampton vilevile iko katika harakati za kumsajili mrithi wa Ronald Koeman aliyeelekea kujiunga na klabu ya Everton hatua ambayo huenda ikachelewesha mpango huo. Klopp alipendezwa na Mane ambaye alihusishwa sana na uhamisho wa Old Trafford wakati wa Louis Van Gaal wakati alipofunga mara mbili baada ya Southampton kutoka nyuma 2-0 na kuiadhibu Liverpool 3-2. Mshirikishe mwenzako Unavyoweza kumshiriki
Sports
Tafadhali Share na marafiki story hiiTimu ya taifa ya soka nchini Ufaransa imeshinda mechi ya ufunguzi wa dimba la kombe la bara Ulaya baada ya kuinyuka Romania, mabao 2-1, katika uwanja wa Stade de France mjini Paris. Dimitri Payet wa Ufaransa ambaye anaichezea klabu ya West Ham nchini Uingereza alifunga bao la ushindi katika muda wa lala salama. Mshambuliaji wa Ufaransa Olivier Giroud alifunga bao la kwanza kwa kichwa muda mfupi tu baada ya kipindi cha pili kung'oa nanga, na baadaye Romania wakazawazisha kwa mkwaju wa penalti kutoka kwa Bogdan Stancu. Image copyrightGETTY Image caption Euro2016 Usalama umeimarishwa mjini Paris na haswa karibu na uwanja wa Stade de France, ambapo shambulizi baya la kigaidi lilitekelezwa mwaka ulopita.
Sports
Tafadhali Share na marafiki story hiiKIPA Benedictor Tinocco atatolewa kwa mkopo, wakati kiungo Salum Abdul Telela hataongezewa Mkataba Yanga. Habari za ndani ambazo BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE imezipata kutoka Yanga zimesema kwamba maamuzi hayo yamepitishwa na kocha Mholanzi, Hans van der Pluijm. “Tinocco atatolewa kwa mkopo sehemu ambayo anaweza kupata nafasi ya kucheza, ili kama atapandisha uwezo wake, anaweza kurudishwa, lakini Telela kocha (Pluijm)” kimesema chanzo kutoka Yanga. Bado haijafahamika haswa sababu za Telela kutoongezewa Mkataba, licha ya umuhimu wake wa wazi unaoonekana katika timu kwa sababu ni kiraka anayeweza kucheza kama beki wa kulia, kati na nafasi zote za kiungo.  http://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js Fundi Salum Telela ameachwa Yanga SC licha ya kwamba bado ni mchezaji muhimu katika timu Na kuhusu suala la nidhamu, Telela anaonekana ni mchezaji mwenye nidhamu, bidii ya mazoezi na kujituma, ambaye wakati wote anapoingizwa uwanjani licha ya muda mwingi kuwa mchezaji wa akiba hucheza vizuri. Wakati huo huo, Yanga inaendelea kusubiri ofa ya kumuuza mshambuliaji Paul Nonga ambaye ameombwa mwenyewe kuuzwa, ili kwenda timu ambayo atakuwa anacheza. Nonga aliyesajiliwa Desemba kwa dau la Sh. Milioni 20 kutoka Mwadui FC ya Shinyanga ameamua kuondoka baada ya kushindwa ushindani wa namba. Washambuliaji chaguo la kwanza wa Yanga ni Mzimbabwe Donald Ngoma na Mrundi, Amissi Tambwe wakati Nonga alikuwa wa akiba pamoja na Malimi Busungu na Matheo Anthony. Tayari Yanga SC imekwishamuacha kiungo kutoka Niger, Issoufou Boubacar ambaye pia alisajiliwa dirisha dogo Desemba.
Sports
Tafadhali Share na marafiki story hii Na Sultani Kipingo Mchakato wa uchaguzi mkuu wa klabu Dar es salaam Young Africans Football Club maarufu kama Yanga ulifanyika kwa utulivu na amani na kumalizika salama jana Jumamosi katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salam na matokeo kamili ni kama ifuatavyo: Mwenyekiti Yusuph Manji (pichani juu) alitangazwa mshindi rasmi wa kiti hicho kwa mara ingine tena baada kuzoa kura zote za ndio isipokuwa mbili tu. Yaani alipata kura 1,468 kati ya 1,470 zilizopigwa huku kura mbili tu zikiharibika. Hakukuwa na kura ya hapana. Manji hakuwa na mpizani kwenye nafasi hiyo. Makamu mwenyekiti Clement Sanga ambaye naye pia alikuwa akigombea nafasi hiyo kwa mara ingine kwa kupambana na Titus Osoro, aliibuka mshindi kwa kujizolea kura 1,428 kati ya 1,508 zilizopigwa. Mpinzani wake aliambulia kura 80 tu. Nafasi za 20 za ujumbe ambazo wagombea waliibuka na ushindi katika uchaguzi huo ni: 1. Siza Augustino Lymo (1027) 2. Omary Said Amir (1069) 3. Tobias Lingalangala (889) 4. Salim Mkemi (894) 5. Ayoub Nyenzi (889) 6. Samuel Lucumay (818) 7. Hashim Abdallah (727) 8. Hussein Nyika (770) Idadi ya wajumbe 12 ambao walishindwa kuibuka na ushindi baada ya kura kutotosha ni: 1. David Luhago (582) 2. Godfrey Mheluka (430) 3. Ramadhani Kampira (182) 4. Edgar Chibura (72) 5. Mchafu Chakoma (69) 6. George Manyama (249) 7. Bakari Malima "Jembe Ulaya" (577) 8. Lameck Nyambaya (655) 9. Beda Tindwa (452) 10. Athumani Kihamia (558) 11. Pascal Lizer (178) 12. Silvester Haule (197) http://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js
Recent Comments