Serikali ya Kenya imefichua kwamba imewakamata raia wanane wa Tanzania waliokuwa katika harakati za kujiunga na kundi la wapiganaji la al-Shabab nchini Somalia.
Katika taarifa iliotumwa katika vyombo vya habari, polisi wanasema raia hao waliokamatwa katika kipindi cha miezi miwili iliopita walikiri kuwa mbioni kujiunga na kundi hilo la ugaidi.
Hatua hiyo inajiri siku chache baada ya kundi la watu wanaojidai kuwa wapiganaji wa Kiislamu kuweka video mtandaoni likidai uwepo wa wapiganaji wa Kiislamu nchini Tanzania
Video hiyo iliwaonyesha wanaume hao wakiwa wamejifunika nyuso zao kwa vitambaa na barakoa.
Wanadai wamo katika mji wa Tanga na kuwahimiza Waislamu katika taifa hilo la Afrika Mashariki kujiunga na kampeni yao.
Wapiganaji wa Kiislamu wadai 'wamo Tanzania'
Polisi wa Kenya pia wanasema wamefanikiwa kutibua njama ya wanachama wa kundi linalojiita Islamic State ya kutekeleza mashambulio nchini humo na kuwakamata washukiwa wawili.
Wawili hao Kiguzo Mwangolo Mgutu na Abubakar Jillo Mohammed walipewa mafunzo ya kuwa na itikadi kali kabla ya kuingizwa katika kundi la IS na Mohammed Ali aliyekamatwa awali na ambaye anasaidia polisi na uchunguzi, polisi wamesema.
Kulingana na taarifa hiyo, kufuatia kukamatwa kwa Mohammed Ali, wafuasi wake wamekuwa wakipanga kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi sana wakilenga sekta ya uchukuzi wa abiria.
Kukamatwa kwa wawili hao, kumezuia kutokea kwa mashambulio katika miji ya Nairobi na Mombasa.
Mshirikishe mwenzako Unavyoweza kumshirikisha m
News
Tafadhali Share na marafiki story hii
zamani wa Myanmar Thein Sein
Mwaandishi mmoja nchini Myanmar amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela, baada ya kutunga shairi kwa kuchora sura ya Rais wa zamani wa Myanmar, Thein Sein kwenye uume wake.
Maung Saungkha amehukumiwa kwa kosa la kumharibia mtu sifa mtandaoni baada ya kuchapisha shairi hilo katika mtandao wake wa kijamii wa Facebook.
Sasa akifahamika kama "penis poet", mtu huyo mwenye umri wa miaka 24 ataachiliwa huru baada ya kutumikia kifungo hicho cha miezi sita gerezani.
Mamlaka kuu nchini Burmer, inaendelea kuwafunga raia wake jela kwa kutoa maoni kwenye mitandao ya kijamii, ambayo yanaikosoa serikali hiyo.
News
Tafadhali Share na marafiki story hii
Wizara ya maswala ya kigeni nchini China imekana ripoti kwamba kampuni za chakula nchini humo zinaweka nyama ya binaadamu na kuuza barani Afrika kama nyama ya ng'ombe.
Chombo cha habari nchini humo Xhinua kimesema kuwa jarida moja nchini Zambia lilimnukuu kimakosa mwanamke mmoja ambaye hakutajwa anayeishi China.
Alisema kuwa kampuni za China zilikuwa zikichukua miili ya wafu kuitia katika viungo na kuiweka katika mikebe.
Msemaji wa China Hong Lei amesema kuwa ripoti hizo hazina uwajibikaji.

Image caption
Nyama ya mkebe kutoka China
Balozi wa China nchini Zambia,Yang Youming ,amesema kuwa ripoti hizo zililenga kuharibu uhusiano mzuri kati ya mataifa hayo mawili.
''Leo jarida moja linasambaza uvumi ,likidai China inatumia nyama ya binaadamu ambayo uihifadhi katika mikebe na kuiuza Afrika.
''Hii ni dhulma ya makusudi ambayo haiwezi kukubalika kabisa kwetu sisi''.
Mshirikishe mwenzako Unavyoweza kumshirikisha mwenzako
Facebook
News
Tafadhali Share na marafiki story hii
VYAMA vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) leo imeivua nguo Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) bungeni, anaandika Regina Mkonde.
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni imeeleza kwamba, Serikali ya CCM ina ufundi wa kupanga mipango mingi lakini haina uwezo wa kutekeleza na kwamba, kinachofanywa ni kudanganya wananchi.
Moja ya mambo yanayoonekana kukera upinzani ni pamoja na Serikali ya CCM kutotoa fedha za miradi kwa wakati jambo linalosababisha kukwama kwa mipango iliyopangwa.
Hayo yamesema na Wilfred Lwakatare wakati akitoa hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni leo mjini Dodoma kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.
“Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ilitengewa fedha iliyokuwa imeombwa na kupitishwa na Bunge katika mwaka wa fedha 2015/2016. Hata hivyo kutokana na sababu ambazo Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni haikuweza kuzifahamu, fedha zilizotengwa hazikuweza kutolewa kama ambavyo ilipangwa na kusababisha kukwama kwa mipango iliyokuwa imepangwa kufanyika,” amesema.
Lwakatare amesema, sababu ya kutotolewa fedha za miradi mapema na kwa wakati ni kitendo cha Serikali ya CCM kupanga mipango mingi kila mwaka na kwamba utekelezaji wake umekuwa duni.
“Mtiririko mkubwa na ahadi na mipango chungu nzima niliyoitaja na nyingine niliyoiacha ambayo ilipangwa na kuahidiwa na Wizara kutekelezwa katika kipindi cha Bajeti ya mwaka 2015/2016, utekelezwaji wake ndicho kinapaswa kuwa kipimo pekee cha utendaji wa Wizara hii,” amesema.
Amesema, serikali haina budi kutoa fedha za kutosha kwenye wizara hiyo kwa kuwa, ina majukumu mengi hasa kutokana na ongezeko la wananchi wengi wenye uhitaji wa huduma zitolewazo na wizara hiyo.
“Majukumu ya Wizara hii ni makubwa na kuna ongezeko la wananchi waliowengi wanaohitaji huduma zaidi kutoka Wizarani.
“Katika mipango ya bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017, wizara imetengewa fedha ndogo zaidi ukilinganisha na fedha zilizokuwa zimetengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2015/2016 ambacho ni kiasi cha shilingi 72,356,901,000/=ukilinganisha na kiasi cha shilingi 61,827,711,000/ kwa mwaka wa fedha 2016/2017,”amesema.
Lwakatare amesema kuwa bajeti iliyotengwa haitakidhi mahitaji ya wizara ya ardhi hasa kwa fungu dogo lililotengwa kwa ajili ya matumizi mengine(OC) na kwamba fungu hilo halitoshi kusimamia mipango ya maendeleo.
“Kwa jinsi bajeti ilivyotengwa ni maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuwa hali hii ni kuonyesha kujikwaa kabla ya safari kuanza. Fungu la OC ambalo limetengewa kiasi cha Tshs. 2,548,492,000 pekee ni dogo mno kuweza kusimamia mipango ya maendeleo,” amesema.
Amesema, licha ya fungu la matumizi mengine kugeuzwa kichaka cha kuendeshea ufisadi, ubadhirifu na matumizi yasiyo na tija, serikali inatakiwa kuendelea kutoa fungu hilo kwa kuwa miradi ya maendeleo husimamiwa na kuratibiwa na fungu hilo.
“Ni kweli kuwa kipindi cha nyuma fungu hili limekuwa likitumika kama kichaka cha kuendeshea ufisadi, ubadhirifu na matumizi yasiyo na tija. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaona kuwa inapofikia hata kmaeneo muhimu yakanyimwa fungu hili, swali linabaki kwamba hiyo pesa inayoelekezwa kwenye miradi ya maendeleo itasimamiwa na kuratibiwa vipi?” amehoji.
News
Tafadhali Share na marafiki story hii
SIRI kuu ya James Rugemalira, kumwaga mabilioni ya shilingi kwa baadhi ya majaji wa mahakama kuu, viongozi waandamizi serikalini na madhehebu ya kidini, wabunge na viogogo wa Ikulu, zimeanza kufumuka.
Nyaraka mikononi mwa gazeti hili zinaonesha zaidi ya asilimia 90 ya wale waliopewa fedha na Rugemalira, ni wale waliomsaidia “kufanikisha ukwapuaji wa zaidi ya Sh. 324 bilioni kutoka Benki Kuu (BoT) na kujinasua katika mikono ya sheria.”
“Rugemalira alishika kila mmoja. Kuanzia Ikulu ya Jakaya Kikwete, TAKUKURU, mahakama, BoT, hazina, ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali, viongozi wa madhehebu ya kidini na hata baadhi ya mawaziri wa zamani wenye ushawishi serikalini,” ameeleza kiongozi mmoja mwandamizi kutoka Ikulu.
Amesema, “…fedha katika akaunti ya Escrow zilihusisha mtandao mpana ulioratibiwa na Rugemalira na Harbinder Sigh Seth (Singasinga).”
Majaji wa mahakama kuu, Aloycious Mujulizi na Eudeus Ruhangisa, ni miongoni mwa waliokuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na Rugemalira; na walikuwa washauri wake wakuu wa kisheria.
Mawasiliano kati ya Jaji Mujulizi na Jaji Ruhangisa yalifanyika kupitia kwa Rugemalira mwenywe na katika eneo jingine kupitia kwa mkewe, Benedicta.
Jaji Mujulizi na Jaji Ruhangisa walitajwa bungeni na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), kuwa miongoni mwa vigogo waliopewa mgawo wa fedha hizo na Rugemalira.
Bunge liliagiza majaji hao wachunguzwe na wachukuliwe hatua za kinidhamu na kisheria.
Hadi sasa, hakuna taarifa zozote kuwa majaji walichunguzwa na kuchukuliwa hatua.
Rugemalira alikuwa akimiliki asilimia 30 ya hisa katika kampuni ya kigeni ya IPTL kupitia kampuni yake ya VIP Engineering and Marketing Limited.
Jaji Mujulizi na Ruhangisa walilipwa na Rugemalira kila mmoja Sh. 404 milioni.
Mabilioni ya shilingi yaliyohifadhiwa katika akaunti ya Escrow yalikwapuliwa na Harbinder Sigh Seth, aliyejiita mmiliki wa IPTL kwa msaada mkubwa wa Rugemalira na kile kilichoitwa, “amri ya mahakama.”
Seth alidai kumiliki IPTL kupitia kampuni yake ya Pan African Power Tanzania Limited (PAP).
MwanaHALISI linaweza kuthibitisha kuwa kati ya tarehe 13 na 26 Novemba 2014, kilikuwa kipindi ambacho Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), ilimhoji Rugemalira juu ya ukwapuaji wa fedha katika akaunti ya Escrow.
Aidha, ni katika kipindi hichohicho, Rugemalira alikuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na Jaji Mujulizi na Ruhangisa.
Wengine waliokuwa na mawasiliano na Rugemalira katika kipindi hicho, ni waziri wa nishati na madini, Prof. Sospeter Muhongo; aliyekuwa waziri wa mambo ya nje na uhusiano wa kimataifa, Bernard Membe na aliyekuwa katibu mkuu wa wizara hiyo, Eliakimu Maswi.
Aliyepata kuwa waziri wa utawala bora, Mathias Chakawe; aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU, Edward Hoseah; aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali (AG), Frederick Werema na aliyekuwa waziri wa viwanda na biashara, Dk. Abdallah Kigoda, walikuwa pia na mawasiliano na Rugelalira.
Wengine ni naibu gavana wa BoT, Dk. Enos Bukuku; aliyekuwa Mnikulu Mkuu wa Ikulu, Shaban Gurumo; aliyekuwa Kamishna mkuu mamlaka ya mapato (TRA), Rished Bade na aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali wakati wa ujio wa IPTL nchini (1994), Andrew Chenge.
Orodha ya waliokuwa katika mawasiliano na Rugemalira inahusisha pia mawaziri wa zamani, Paul Kimiti na Wilson Masilingi; aliyekuwa mhariri mtendaji wa magazeti ya serikali – Daily News na Habari Leo – Gabriel Nderumaki; aliyewahi kuwa waziri wa nishati na madini, Wiliam Ngeleja na mkurugenzi wa kampuni ya G and S Consultancy Limited, Dk. Gideon Shoo.
Wengine ni aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Constantine Massawe; Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Methodius Kilain; Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Eusebius Nzigilwa na aliyekuwa waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Prof. Anna Tibaijuka.
Prof. Tibaijuka alikiri kupokea kiasi cha Sh. 1.6 bilioni kutoka kwa Rugemalira. Hata hivyo, alisema kuwa fedha ambazo alipokea zilikuwa ni mchango wa shule yake ya Barbro Johanssen ya jijini Dar es Salaam na Kajumulo Girls High School iliyoko Bukoba.
Kwa mujibu wa taarifa, Dk. Hoseah alimruhusu Rugemalira kutafuta msaada popote pale, ikiwa ni pamoja na nje ya nchi na kwamba ofisi yake “ingetoa maofisa kumsaidia.”
“Kama una jambo la msingi kufanya nje ya nchi, una baraka zangu zote. Watakapohitajika maofisa wa TAKUKURU kwa ufafanuzi, wako tayari kukusaidia pale uliko,” anaeleza Dk. Hoseah na Rugemalira andishi lake la 16 Novemba 2014.
Dk. Hoseah anamaliza kwa kumueleza Rugemalira, “…nakutakia kila la kheri.”
Rugemalira alikuwa anaomba TAKUKURU kuingilia kati kile kinachoitwa, “mgogoro wa hisa kati ya IPTL na Benki ya Standard Chartered (SCB) ya Uingereza.”
Hata hivyo, Rugemalira anaonywa na Masilingi, ambaye wakati huo alikuwa balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, kuwa mwangalifu na mtulivu wakati suala hilo linaendelea.
Alisema, “mimi nikiwa mwanasheria, ninakushauri wewe na kampuni yako kushirikiana kwa ukamilifu na TAKUKURU. Suala la IPTL ni gumu. Limekuwa na mchanganyiko mkubwa. Akili nyingine haziwezi kulielewa.”
Masilingi anasema, “…nimebaini kwamba TAKUKURU ndio wanaolichukulia suala hilo kwa usiri mkubwa katika hatua za uchunguzi na wenyewe wanaweza kukusaidia kupata hukumu iliyo ya haki.”
Benki ya Standard Chartered ilikuwa inadai na mpaka sasa bado inadai kuwa mitambo ya kuzalisha umeme ya IPTL na fedha zilizopo kwenye akaunti ya Escrow, ni mali yake.
Inadai kuwa kampuni ya MECHMAR ya Malasia ilishindwa kurejesha mkopo iliochukua benki na kwamba hilo ni jambo linalosababisha mitambo ya IPTL iliyopo Tegeta Salasala, jijini Dar es Salaam, kuwa mali yake.
Akihutubia taifa kupitia wazee wa mkoa wa Dar es Salaam, wiki tatu baada ya Bunge kuagiza waliohusika katika wizi wa fedha za Escrow wachukuliwe hatua, aliyekuwa Rais wa Jamhuri, Jakaya Mrisho Kikwete alikiri kuwapo udanganyifu katika kufikia utoaji wa fedha hizo.
Alikiri baadhi ya nyaraka kughushiwa. Akakiri kuwa kampuni ya PAP imekwepa kodi ya serikali na kudai kuwa serikali yake bado inaendelea kuitafuta kampuni ya MECHMAR iliyodaiwa kuuza asimia 70 ya hisa zake ndani ya IPTL.
Rais alikiri kuwa aliyepewa fedha na serikali – PAP – hakuwa na sifa; serikali yake haikufanya uchunguzi yakinifu kuhusu historia, uhalali, sifa na uwezo wa kampuni ya PAP katika uwekezaji wa umeme, ununuzi wa mitambo na mtaji.
Naye mwanasheria wa Rugemalira, Camilo Schutte, katika barua aliyomwandikia Rugemalira, anasema “…baada ya kusoma ushauri wa Masilingi juu ya msaada wa TAKUKURU, itakuwa busara kuomba TAKUKURU kusubiri hukumu kati ya Standard Chartered na IPTL.”
Anasema kampuni ya Rugemalira (VIP) “…inapaswa kuomba TAKUKURU kufanya uchunguzi juu ya sera ya benki ya Standard Chartered kuhusu ununuzi wa madeni ambayo mchakato wake unaweza kuwa na rushwa.”
Camilo Schutte anamueleza Rugemalira katika barua yake hiyo na ambayo imenakiriwa kwa majaji, mawaziri, kiongozi wa TAKUKURU, maofisa wa Ikulu na watu wengine kuwa, “…tatizo la benki ya Standard Chartered, kama zilivyo taasisi nyingine, ni kufanya biashara ili kujipatia faida kubwa.”
Akiandika kwa Dk. Gideon Shoo, mwanasheria wa Rugemalira (Camilo Schutte) anaelekeza kufanyika mambo matatu kwa haraka.
Kwanza kutafuta, kwa “gharama yoyote ile,” watu wote wenye ushawishi mkubwa kwenye jamii ambao wanapigia kelele ukwapuaji wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.
Miongoni mwa waliotajwa, ni Zitto Kabwe, mbunge wa sasa wa Kigoma Mjini; David Kafulila, ambaye alikuwa mbunge wa Kigoma Kusini; Balozi wa Uingereza nchini, Dianna Melrose; Wilson Masilingi na balozi wa Finland nchini.
Pili, Camilo Schutte anasema, ni sharti mtandao wao ujiridhishe ikiwa watu wanaolizungumzia jambo hilo wanalifahamu kwa undani au wanalijua nusunusu au hawalijui kabisa.
Kwa maoni ya mwanasheria wa Rugemalira, wabunge waliokuwa wameshupalia jambo hilo walikuwa hawana taarifa zozote muhimu kuhusu suala hilo.
Tatu, mwanasheria alimtaka Dk. Shoo kuangalia athari za taarifa zilizosambazwa juu ya ukwapuaji wa fedha hizo, kwa kampuni ya IPTL na Rugemalira binafsi.
“Baada ya kukamilisha haya, naomba unijulishe haraka ili tuweze kupanga mikakati ya kukabiliana na kila tatizo nililolitaja hapo juu,” anaeleza Camilo Schutte.
Kupatikana kwa mawasiliano haya kumekuja mwaka mmoja na nusu baada ya mabilioni ya shilingi kukwapuliwa BoT; na Bunge kuelekeza serikali kufanya uchunguzi.
Aidha, kupatikana kwa taarifa kuwa Rugemalira alikuwa na mawasiliano ya karibu na “kindungu” na mkuu wa TAKUKURU, kumekuja wakati ambapo taasisi hiyo imeshindwa kuanika orodha ya watu walionufaika na mgawo wa fedha hizo kutoka benki ya Stanbic.
Bunge liliagiza serikali kufikisha mahakamani watuhumiwa wote wa Escrow, ikiwa ni pamoja na kufilisi mtambo wa IPTL na kuitangaza benki ya Stanbic kuwa taasisi ya kutakatisha fedha.
Bunge liliagiza pia kuchunguza na kuwajibisha majaji waliotajwa kunufaika na mgawo wa fedha kupitia benki ya Mkombozi na kumfukuza nchini, anayejiita mmiliki wa IPTL, Harbinder Sigh Seth.
Akizungumzia kutajwa kwa Dk. Hoseah na baadhi ya majaji katika mawasiliano na Rugemalira, mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu amesema jambo hilo linaongeza shaka juu ya uadilifu wa viongozi wa CCM na serikali yake.
Ameliambia gazeti hili katika mahojiano kwa njia ya simu, “…hili liserikali lote limeoza. Kuanzia Ikulu, mfumo wa mahakama hadi viongozi wa madhehebu ya kidini; kote kumejaa rushwa.”
Lissua ameongeza, “Tulisema ndani ya Bunge, kwamba majaji wamehongwa na hivyo tukataka wachunguzwe, lakini serikali ya CCM imegoma kwa kuwa walioiba waliwajua na walishirikiana nao.”
Mwanasiasa huyo wa upinzani anasema, “utapeli huu ulifanywa na serikali ya Rais Kikwete, BoT, Benki ya Stanbic na PAP.”
Amesema, “…sasa kama kweli wanataka kusafisha nchi, basi waanzie hapo. Siyo kukimbizana na vidagaa. Waanze na maofisa wao wa Ikulu waliokuwa wameigeuza ofisi ya umma kuwa ofisi binafsi.”
Gazeti toleo lenye makala hii
News
Tafadhali Share na marafiki story hii
Kwa mara nyingine jana wakazi wa Jiji la Tanga walikumbwa na taharuki baada ya kijana mmoja kurusha bomu la mkono chini ya daraja wakati wananchi walipokuwa wakimfukuza baada ya kukurupushwa na polisi.
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Leonard Paulo alisema kijana huyo alikurupushwa na askari waliokuwa kwenye msako wa kuwatafuta majambazi waliofanya mauaji Aprili 20, mwaka huu katika duka la Central Bakery.
Alisema tukio hilo lilitokea juzi saa mbili usiku kwenye Mtaa wa Makora, Tarafa ya Ngamiani.
Awali, Kamanda Paulo alisema kijana huyo anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 25 na 30, alipokurupushwa alianza kutimua mbio.
“Alipoanza kukimbia ndipo wananchi wakaingilia kati, walimfukuza na kumshambulia kwa mawe huku wakimpiga na kitu chenye ncha kali kisogoni, ndipo wakati akipelekwa Hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo akafariki dunia njiani,” alisema Kamanda Paulo.
Mapema kabla hajafariki dunia, kamanda alisema kijana huyo alipokurupushwa alikimbia akiwa ameshikilia bomu mkononi.
Kamanda aliwataka wakazi wa Tanga kuwa watulivu kwa sababu vyombo vya dola viko katika operesheni maalumu ya kuwasaka walioshiriki mauaji ya hivi karibuni katika hilo la mikate.
Walioshuhuda tukio hilo walisema kijana huyo alishambuliwa na wananchi baada ya kukwapua simu ya mwanamke mmoja katika Mtaa wa Makorora.
Walisema alianza kukimbia na alipoona wananchi wanamfukuza aliwatahadharisha kuwa wakimsogelea atarusha bomu alilokuwa amelishika mkononi.
Kufuatia kutishiwa na bomu hilo, wananchi waliokuwa wakimkimbiza walipiga simu Kituo Kikuu cha Polisi cha Chumbageni kwa ajili ya kupatiwa msaada.
“Kwa hili tunawapongeza polisi. Walitumia dakika chache kufika eneo la tukio lakini walipobaini kwamba ni bomu, wakaamua kuwasiliana na maofisa wataalamu wa kutegua mabomu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi (JWTZ) ambao waliwasili eneo la tukio,” alisema Rajabu Hamis.
Wakizungumza kuhusu tukio hilo, baadhi ya wakazi wa Tanga waliomba vyombo vya ulinzi na usalama kuimarisha ulinzi kwa sababu wamejawa na hofu, kwa kuwa matukio yanayohatarisha amani yanazidi kutokea.
“Hii ni changamoto kwa vyombo vya ulinzi na usalama, matukio haya yanazidi kuwapa hofu wananchi. Mwezi uliopita yalifanyika mauaji makubwa Central Bakery, leo bomu tena,” alisema Kassim Mbughuni.
News
Tafadhali Share na marafiki story hii
But Mr Trump faces a huge task in trying to get the Republican party behind him, as doubts persist about his substance and style.
House Speaker Paul Ryan, the party's highest-ranking elected official, has said he is unable to endorse the New York businessman because he lacks conservative principles.
West Virginia results as they come in
Nebraska Republican results as they come in
Why Bernie Sanders is still running
Who will be Trump's running mate?
Trump v Republicans - the gulf between
Anthony Zurcher, BBC News, Washington
With victories in Indiana and now West Virginia, Bernie Sanders has started another winning streak against Hillary Clinton. Like his five-state run in April, however, it will do little to slow her steady march to the Democratic nomination.
Exit polls show the West Virginia vote was particularly quirky. Almost 40% of Democratic voters there said they wanted a president less liberal than Barack Obama - and that group favoured avowed socialist Sanders by more than a two-to-one margin.
Mr Sanders also overwhelmingly carried the 27% who want a president more liberal than Mr Obama.
Such a result makes sense if some of Sanders's support is, in fact, an anyone-but-Clinton vote.
At this point the Vermont senator will likely take help wherever he can get it. He should be competitive in the next four contests, but could hit a wall in the June mega-prize, California. Its diverse electorate favours Mrs Clinton, and anything but an unprecedented Sanders win there would seal his fate.
Until then, however, Mr Sanders will continue to be a constant and unpleasant reminder to Mrs Clinton that there are Democratic voters still unwilling to fully get on board her campaign.
News
Tafadhali Share na marafiki story hii
A car bomb at a crowded market in northern Baghdad has killed at least 64 people and wounded 87 others, Iraqi police and medical sources say.
It happened at the Shia district of Sadr City during the morning rush hour.
So-called Islamic State (IS) said it had carried out the attack, targeting Shia militiamen.
The mainly Sunni group, which controls swathes of northern and western Iraq, has frequently targeted Shia, whom it considers heretics.
Many of the victims included women and children, officials said. Several of the injured were said to be in critical condition.
The blast damaged nearby buildings and other vehicles.
Battle for Iraq and Syria in maps
Islamic State group: The full story
Image copyrightREUTERS
Image caption
The attack targeted a busy market in a Shia district in northern Baghdad
Image copyrightREUTERS
Image caption
It happened during a busy period in the morning
IS has frequently targeted commercial areas and government and security personnel, causing heavy casualties.

Recent IS deadly bombings
March 2016: Suicide attack in a football match in the city of Iskandariya, in central Iraq, kills at least 32 people. Many of the dead are young boys who were in a trophy ceremony.
March 2016: Fuel tanker is blown up at a checkpoint near Hilla, south of Baghdad, killing at least 47 people.
February 2016: Twin suicide bomb attack in a busy market in Sadr City kills at least 70 people.

Iraqi forces, backed by US-led coalition air strikes and Shia-dominated paramilitary forces, have regained some territory seized by IS in 2014, but have been unable to prevent bomb attacks in the capital.

News
Tafadhali Share na marafiki story hii
Subscribe to:
Posts (Atom)
Recent Comments